DAR ES SALAAM
OPERESHENI Ukuta
iliyotangazwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) itakayokwenda
sambamba na mikutano ya hadhara na maandamano nchi nzima kuanzia Septemba Mosi,
imezua taharuki miongoni mwa makundi mbalimbali nchini.
Akitangaza uamuzi
huo juzi Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alisema
operesheni hiyo ina lengo la kuzuia matukio ya ukandamizaji wa haki na
demokrasia aliyoda kuwa yanafanywa na Rais Dk. John Magufuli dhidi ya makundi
mengine ya kisiasa na kijamii.
Mbowe alisema
Kamati Kuu ya chama hicho imeainisha hoja 24 za chimbuko la Ukuta (Umoja wa
Kupambana na Udikteta Tanzania), mojawapo ikiwa ni hatua ya Rais Magufuli
kupiga marufuku mikutano yote ya hadhara ya vyama vya siasa hadi mwaka 2020.
Siku moja baada ya
tamko hilo, Msajili wa vyama vya siasa nchini, jaji Francis Mutungi ametoa
taarifa ya kulaani tamko hilo la Chadema akisema limejaa lugha ya uchochezi,
kashfa, kuudhi na linahamasisha vurugu na uvunjifu wa amani.
Kwa upande wake,
Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimeitaka Chadema kuzingatia sheria kwa kutii zuio
la mikutano ya hadhara lililotolewa na Jeshi la Polisi.
Akizungumza na
waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Msemaji wa CCM, Christopher ole
Sendeka, amesema Chadema wanapotosha umma kwani Serikali haijazuia mikutano ya
kikatiba kwenye majimbo yao.
Wakati Sendeka akisema
hivyo, wabunge wa Chadema, Wilbroad Qambalo (Karatu) na Cesilia Pareso (Viti
Maalumu), walihojiwa juzi na Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha kwa kosa la kufanya
mikutano na wananchi bila kibali cha polisi.
Mbali na Chadema,
taarifa ya ziara zinazotarajiwa kufanywa na Rais Magufuli, ambaye pia ni
mwenyekiti wa CCM, Singida na Kahama mkoani Shinyanga kwa lengo la kuwashukuru
wananchi kumpigia kura Oktoba mwaka jana, imepokewa kwa hisia tofauti na baadhi
ya wasomi, viongozi wa dini na wananchi wa kawaida.
Baadhi ya
wachambuzi wa siasa na baadhi ya viongozi wa dini waliozungumza wamesema
kitendo cha rais kuzuia vyama vya upinzani kufanya mikutano wakati yeye
akifanya mikutano kimetokana na udhaifu wa katiba ya mwaka 1977 inayotumika
sasa.
GEITA
WAZIRI wa Mambo ya
Ndani, Mwigulu Nchemba, amefanya ziara ya kushtukiza katika Mgodi wa Dhahabu wa
Nyamahuna mkoani Geita na kukuta Wachina 72 kati ya 100 wakiishi na
kufanya kazi bila vibali.
Akizungumza katika
mgodi huo unaomilikiwa na Mtanzania, Andrew Obole, Mwigulu amesema alifika hapo
kutokana na kuona taarifa zilizozagaa kwenye mitandao ya jamii zikimuonyesha
Masanja Shokera akicharazwa bakora na raia wa mmoja wa China, Lee Swii, kwa
madai ya kuiba mawe ya dhahabu Julai 6, mwaka huu.
Amesema taarifa
alizonazo ambazo zipo uhamiaji zinaonyesha kuwa raia wa China waliopo mgodini
hapo ni 28 ambao wana vibali halali vya kuishi nchini.
Waziri amesema kwa
sababu hiyo, ameagiza Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Geita kuwaweka
chini ya ulinzi Wachina wengine 72, walinzi saba na Kaimu Meneja Uzalishaji,
Richard Joachim.
Vilevile
huyo anayeitwa Lee ambaye anatuhumiwa kumdhalilisha Mtanzania ameamriwa awekwe
chini ya ulinzi na walinzi saba.
Masanja Shokera
anayedaiwa kudhalilishwa, , amesema siku hiyo alivamiwa na walinzi
wa mgodi huo akituhumiwa kuiba mawe ya dhahabu.
Amesema walimpiga
na kumfunga mikono na miguu na kuendelea kumwadhibu hali iliyosababisha
apoteze fahamu.
Mkurugenzi wa mgodi
huo, Andrew Obole amesema anachotambua Wachina waliopo kwake ni 28 na kwamba
hao wengine alikuwa hawatambui.
DAR ES SALAAM
KITUO cha Sheria
na Haki za Binadamu (LHRC) kimezindua Ripoti ya Haki za Binadamu na Biashara
kwa Mwaka 2015 ambacho kimebainisha kuwa asilimia 60 ya wafanyakazi nchini
hawana Mikataba stahiki ya kazi, jambo linalosababisha serikali kupoteza mapato
ya kodi.
Aidha ripoti imebainisha
Mikataba mingine iliyopo kuwa na upungufu mwingi ikiwa ni pamoja na miongoni
mwao kuandikwa kwa lugha isiyoeleweka na mingine kuandikwa kwa ufupi na
kushindwa kujumuisha mambo ya msingi.
Nalo Shirikisho la
Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA), limekiri kuwepo kwa matatizo hayo kwa
wafanyakazi lakini likafafanua kuwa wengi ni waoga kufukuzwa kazi, hivyo
wanashindwa kujitokeza hadharani na kueleza yanayowasibu.
Akizungumzia
ripoti hiyo wakati wa uzinduzi jijini Dar es Salaam jana, Mtafiti wa Taarifa wa
LHRC Clarence Kipobota amesema miongoni mwa wafanyakazi ambao wamekuwa
wakifanya kazi kwa kukosa Mikataba halali ya kazi ni pamoja na waandishi wa
habari pamoja na madereva.
Amesema kutokuwepo
pia kwa vyama vya wafanyakazi katika maeneo ya kazi, kumekuwa kukichangia wengi
wao kukosa makubaliano ya pamoja.
DODOMA
RAIS John Magufuli
ametengua uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Barabara Dk James Wanyancha.
Taarifa ya Katibu
Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi iliyotolewa mjini Dodoma jana imesema Rais
Magufuli ametengua uteuzi huo kuanzia Julai 28, 2016.
Imesema kufuatia
kutenguliwa kwa uteuzi huo, Rais Magufuli amemteua Joseph Odo Haule kuwa
Mwenyekiti mpya wa Bodi hiyo.
Kwa mujibu wa
taarifa hiyo ya Balozi Kijazi, uteuzi wa Haule umeanza jana Julai 28.
Kabla ya uteuzi
huo Haule alikuwa Meneja wa Mfuko wa Barabara. Wajumbe wengine wa Bodi ya Mfuko
wa Barabara wanaendelea katika nafasi zao.
KIONGOZI wa Kanisa
Katoliki Duniani, Papa Francis (79) jana alianguka wakati wa ibada,
kwenye madhabahu ya Jasna Gora, mjini Czestoshowa, Poland.
Tukio hilo
lilitokea baada ya Papa Francis kujiikwaa akiwa madhabahuni hali
iliyowalazimu mapadre waliokuwa karibu naye kumsaidia kuinuka.
Taarifa zinasema
Papa alianguka chini karibu na ngazi za madhabahuni na aliinuliwa na mapadri
waliokuwa kwenye misa hiyo.
Kwa mujibu wa
taarifa za utabibu, Papa Francis amekuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa sciatica
unaosababishwa na maumivu chini ya mgongo.
Papa Francis,
ambaye ni mzaliwa wa Argentina alionekana akitembea huku akitafakari
hali iliyomfanya asigundue kuwa kulikuwa na ngazi mbele yake.
Baad ya kuinuka,
Papa Francis, aliendelea na taratibu za ibada kama ilivyopangwa.
Alihubiri kwa muda
mrefu kwenye ibada hiyo iliyohudhuriwa na maelfu ya waumini huku ikifuatiliwa
pia na mamilioni ya waumini wa dhehebu hilo, kwa njia ya runinga.
Msemaji wa
Vatican, Greg Burke, aliwaambia waandishi wa habari kuwa kiongozi
huyo yuko salama na hakuna maumivu yoyote aliyoyapata alipoanguka.
Papa Francis
aliwahi kuteleza na hata kuanguka mara kadhaa na kila mara huwa
anainuka peke yake au kusaidiwa na mmoja wa wasaidizi wake,
Kiongozi huyo wa
Kanisa Katoliki Duniani aliendesha ibada katika kituo cha utawa
ambayo ni nyumba maarufu ya watu kale kwa Kanisa Katoliki.
Katika ibada hiyo,
ulinzi ulikuwa mkali kutokana muendelezo wa mashambulio ya ugaidi barani Ulaya.
Wanajeshi na
polisi walionekana maeneo mbalimbali ya barabara katika ziara hiyo ya siku tano
nchini Poland.
Hillary
Clinton amekubali rasmi kuwa mgombezi wa Urais wa Marekani kupitia chama cha
Democratic, huku akisema wakati wa kupambana na mpinzani wake sasa umeanza
rasmi.
Alitoa
wito kwa wanachama wote wa Democratic kuungana naye huku akimkebehi mpinzani
wake wa chama cha Republican, Donald Trump, katika madai yake kuwa ni yeye
pekee anayeweza kuyasuluhisha matatizo ya Marekani.
Alisema
kuwa Wamarekani hufanya kazi kwa pamoja kyatatua yote yanayonufaisha taifa.
Awali,
bintiye Chelsea Clinton alikuwa ametoa hotuba na kumsifu sana mamake. Alisema
ni mwanamke ambaye huwa hasahau anawapigania akina nani.
"Watu
huniuliza kila wakati, huwa anawezaje kufanya haya? ... ni kwa sababu huwa
hawasahau watu anaowatetea," amesema.
"Najua
kwa moyo wangu wote kwamba mamangu atatufanya tujionee fahari."
Mke
wa mgombea urais wa chama cha Republican nchini Marekani Donal Trump, Melania,
amefuta tovuti yake baada ya vyombo vya habari nchini Marekani kuanza kutilia
shaka ukweli wa baadhi ya madai yake.
Bi
Trump amesema tovuti hiyo imefutwa kwa sababu haikuwa inaashiria wala kuonyesha
mambo anayoangazia kwa sasa.
Vyombo
vya habari nchini Marekani vilikuwa vimetilia shaka ukweli wa madai kwamba ana
shahada katika usanifu mijengo kutoka chuo kikuu kimoja nchini Slovenia, kama
alivyokuwa ameandika katika wasifu wake mtandaoni.
Kitabu
kuhusu maisha yake kilichochapishwa mwaka huu kinasema aliacha masomo baada ya
mwaka mmoja kuangazia kazi ya uanamitindo.
Wiki iliyopita,
Melania Trump, alishutumiwa vikali baada ya hotuba aliyoitoa kwenye Kongamano
kuu la chama cha Republican, kudaiwa kuwa kukopa
sana maneno kutoka kwa hotuba iliyotolewa na mke wa rais wa sasa Michelle
Obama katika kongamano la chama cha Democratic miaka minane iliyopita
No comments:
Post a Comment